
Uhusiano na mshindi wa pili wa Miss
Tanzania 2013, Latifa Mohamed wenye miezi tisa sasa, ndio uhusiano mrefu
zaidi aliowahi kuwa nao Ben Pol tangu awe staa.
Ben Pol ameiambia Bongo5 kuwa mahusiano
yake yaliyopita yalishindwa kudumu kwakuwa wasichana wengi walikuwa na
matarajio makubwa kutoka kwake kwakuwa yeye ni msanii. “Sasa hivi tuna
miezi tisa, nadhani ndio the longest relationship,” amesema Ben kuhusu
uhusiano na Latifa.
“Unajua nimekutana na watu wa aina
tofauti. Nimekutana na watu ambao labda wanakuwa na expectations kubwa
zaidi kuhusu mtu fulani, kwahiyo akiingia kwenye maisha yako labda kuna
vitu ambavyo yeye tayari alishapicture,...