Marin Hinkle
Wazazi wake walikutana katika moja ya harakati za kuleta amani
Africa,akazaliwa nchini Tanzania,ila baadae, baada ya familia yao
kumaliza mkataba wa kufanya kazi ,walirudi nchini Marekani mjini
Boston,na ndipo alipokulia na kufanikiwa kwenda kusomea mambo ya sanaa
chuoni.
Huyu ni actress maaruf sana Hollywood,kwa wapenzi wengi wa filamu
wanaweza kumgundua mapema,kupitia movie kadhaa alizowahi kucheza,katika
filamu zilizowahi kuchukua tuzo na kufanya mauzo makubwa sana
duniani.Amewahi kucheza kama starring msaidizi kwenye movie ya Once and
Again,akacheza tena kwenye series maarufu ya Two and half Men na
kuonesha kipaji chake kwenye series nyingine mpya ya Law &
Order:Special Victims Unit.
Rachel Luttrell
Rachel Luttrell ni mcheza filamu na muimbaji maarufu
duniani,alizaliwa hapa hapa Jijini Dar es salaam,Tanzania ,yeye akiwa ni
mtoto wa kike wapili katika familia yao,baba yake akiwa ni professor wa
Economics, katika chuo cha Dar es salaam.Baada tu ya kufikisha miaka
mitano ,yeye na familia yake nzima ikahama nchi nakurudi kwao Canada
katika jiji la Toronto.
Mbali na kipaji chake kizuri sana chauchezaji filamu na kuimba,Rachel
ameweza kuandika story ya movie nyingi sana,na kuweza kusaidia
ku-direct yeye mwenyewe,baadhi ya movie alizowahi kucheza ni
“ER”,”Sleepwalkers”,”Feast of All Saints”,”Imposter”,”Stargate
Atlantis”,”I Wish You Love”,NCIS (America’s number one-rated television
show) na nyingine nyingi.Ameweza kupata jina kubwa sana hapo Hollywood
kwa kazi yake nzuri ya uigizaji.
Manish Patel
Huyu ni producer ,mwandishi na Director anayeheshimika sana huko
nchini uingereza,amezaliwa hapa hapa Tanzania ,kati ya mpaka wa Tanzania
na Zambia.Inasemekana kuwa Manish Patel ni moja kati ya wanaharakati
walioweza kuinua sanaa ya filamu huko uingereza kwa kazi yake
nzuri.Movie zake zimeweza kufika level za kimataifa na kuweza
kuchaguliwa katika tuzo mbali mbali za filamu duniani, zikiwemo tuzo ya
the Cannes Film Festival, Portobello Film Festival, Mumbai Film
Festival, Bite The Mango Film Festival na nyingine nyingi. nakushinda
‘Best Film Award’ for ‘Cash and Curry’ kwenye Portobello Film Festival.
Freddie Mercury
Huyu ni mwimbaji nguli,mzaliwa wa huko Zenji ,Stone
Town,Tanzania.Baada ya kuzaliwa kwake na kukaa kwa muda hapa nchini
Tanzania, wazazi wake wakaamua kumpeleka masomoni nchini India,kwenye
shule binafsi.
Baada ya muda,katika kipindi cha masomo yake, alihamia nchini
uingereza,huko ndipo kipaji chake cha kuimba kilipo onekana,alifanikiwa
kwenda katika chuo cha sanaa,na huko ndipo alipokutana na wanafunzi
waimbaji wenzake waliokuwa kwenye kikundi kilichokuwa kinajiita Smile.
Kundi lilopata umaarufu mkubwa nchini marekani ,kufikia mauzo ya
platinum ya album zao.Baada ya miaka kupita ikaja julikana kuwa Freddie
alikuwa na ugonjwa usiojulikana,jambo lilomsababishia ashinde hospitali
na wakati wowote apatapo nafuu hutoka na kuingia studio ku-record,
haikupita muda sana,aliaga dunia,ikawa pigo kubwa katika ulimwengu wa
muziki .
-Vibe
0 comments :
Post a Comment