Pata Habari Motomoto za Nje na Ndani ya Nchi kwa njia ya E-mail, Andika E-mail yako hapo chini.


Showing posts with label ajali. Show all posts
Showing posts with label ajali. Show all posts

UPDATE:MATUKIO PICHA, MSIKITI WA MTAMBANI KINONDONI WAUNGUA TENA



Wananchi wakisaidiana kuokoa mali za Msikiti wa Mtambani mara baada ya kushika moto uliowahi kuzimwa.



Kikosi cha zimamoto kikiwa eneo la tukio kutoa msaada.



Ulinzi ukiwa umeimarishwa eneo hilo la tukio.

(PICHA ZOTE NA DAR ES SALAAM YETU BLOG)



(Picha hii ni wakati msikiti huo ulipoungua mara ya kwanza Agosti 13, mwaka huu)

MSIKITI wa Mtambani uliyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam umeungua tena kwa moto leo mchana. Hii ni mara ya pili msikiti huo kuungua kwa moto baada ya ile ya awali ya Agosti 13 mwaka huu. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme.

PICHA INATISHA.!! MWANAMKE AANGUKA KWENYE BODABODA NA KUKANYAGWA NA LORI




Mwanamke anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 25 amekufa papo hapo baada ya kudondoka kwenye pikipiki aliyokuwa amepanda na kisha kukanyagwa na gari.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura amesema kuwa ajali hiyo ilitokea jana mchana katika barabara ya Bagamoyo eneo la Tangibovu ambapo gari likiendeshwa na dereva asiyefahamika akitoka kwa Alysykes kuingia barabara ya Bagamoyo, aliigonga pikipiki namba T 505 CTJ Fekon ikiendeshwa na dereva asiyefahamika.
Alisema pikipiki hiyo iliyokuwa ikitokea Mbezi Makonde kwenda Mwenge ilikuwa imempakia mwanamke huyo ambaye baada ya pikipiki kugongwa alianguka chini na kisha kukanyagwa na lori namba T 277 CIL aina ya Tata likiwa na trela namba T 339 CYB lililokuwa katika uelekeo mmoja na pikipiki.

Kamanda alisema mwanamke huyo alikufa papo hapo na mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Mwananyamala huku Polisi wakiendelea kuwasaka madereva waliohusika katika ajali hiyo.

BASI LA SUPER FEO LAGONGA MTI NA KUPINDUKA HUKO SONGEA, WAWILI WAFARIKI NA 30 KUJERUHIWA




Watu wawili wamepoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa baada ya ajali mbaya iliyotokea leo katika eneo la Sanangula nje kidogo ya mji wa Songea mkoani Ruvuma ikilihusisha basi la Super Feo linalofanya safari zake kati ya Songea - Makambako lililoacha njia na kugonga mti.

Chanzo cha ajali hiyo kinadaiwa kuwa ni mwendo kasi.




AJALI ZA MABASI NA MALORI ZATIA HOFU TZ,,,..!! LORI LAPINDUKA NA KUUA DEREVA KATIKA MLIMA SEKENKE MKOANI SINGIDA


Wananchi wakishuhudia lori la saruji lililopinduka na kuua dereva wake leo eneo la Milima ya Sekenke mkoani Singida.
Pichani juu na chini malori mengine ya mizigo yakipita karibu na eneo la tukio.
Moja ya lori likitoa msaada wa kulivuta lori lililopata ajali kutoka bondeni. DEREVA wa lori lililokuwa limebeba saruji kutoka jijini Dar es Salaam kuelekea Mwanza leo amefariki dunia baada ya lori hilo kupinduka eneo la Sekenke mkoani Singida. Watu wengine wanne waliokuwa kwenye lori hilo wamejeruhiwa.

Mmoja wa mashuhuda wa ajai hiyo ameiambia tovuti hii kuwa chanzo cha ajali hiyo ni kufeli breki kwa lori hilo lililokuwa likishuka Milima ya Sekenke na mpaka anaondoka eneo la ajali hiyo bado dereva (marehemu) na mmoja wa watu waliokuwemo aliyekuwa hai walikuwa bado wamenasa kwenye lori hilo.

JINAMIZI LA AJALI LAITESA TANZANIA..!! MABASI YA DAR EXPRESS NA SIMBA MTOTO YAGONGANA...




Pichani ni mabasi mawili ya Simba Mtoto na Dar Express yakiwa yamepigana pasi maeneo ya Muheza Mkoani Tanga mchana huu. Haijafahamika mara moja madhara ya ajali hii wala chanzo chake kwa kuwa ripota wetu hakubahatika kumpata msemaji wa polisi. Hata hivyo Globu ya Jamii inaendelea na juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga kwa taarifa zaidi. Tuendelee kuvuta subira.
 

Copyright © 2013. BONGO STARS LINK - Haki zote zimehifadhiwa
Template Modify by Habarizetuleo TEAM
Proudly powered by MAN DUGX