Pata Habari Motomoto za Nje na Ndani ya Nchi kwa njia ya E-mail, Andika E-mail yako hapo chini.


Home » » MREMBO HAMISA MABETO AMUANIKA MCHUMBA WAKE

MREMBO HAMISA MABETO AMUANIKA MCHUMBA WAKE

MAHABA niue! Mwanadafada ambaye ni mwanamitindo Bongo, Hamisa Mabeto ameamua kumwanika mwandani wake baada ya kumuweka kwenye mitandao ya kijamii  huku akimmwagia sifa kemkem.
Mwanadafada ambaye ni mwanamitindo Bongo, Hamisa Mabeto akila ujana na mpenzi wake.
Akipiga stori na mwandishi wa gazeti hili baada ya kuvutiwa waya, Hamisa alisema mwanaume huyo ni mtu ambaye anampenda sana na wana malengo ya kuoana muda wowote kuanzia sasa na jina lake ataliweka hadharani soon!
Aliendelea kusema kuwa wana miezi sita mpaka sasa na amekuwa mtu ambaye anajua nini thamani ya mapenzi kwani muda wowote akimuhitaji anakuwa karibu yake.
Mtoto mzuuuuri... kunako fani ya mitindo Bongo, Hamisa Mabeto akipozi.
“Ni kweli ni mpenzi wangu ambaye tunapendana sana na muda wowote kuanzia sasa tutafunga pingu za maisha kama mipango yetu ikikaa vizuri,” alisema Hamisa.

0 comments :

Post a Comment

 

Copyright © 2013. BONGO STARS LINK - Haki zote zimehifadhiwa
Template Modify by Habarizetuleo TEAM
Proudly powered by MAN DUGX