Pata Habari Motomoto za Nje na Ndani ya Nchi kwa njia ya E-mail, Andika E-mail yako hapo chini.


Home » » Wasanii waosha magari kusaidia waathirika wa ajali za magari Muhimbili

Wasanii waosha magari kusaidia waathirika wa ajali za magari Muhimbili

Wasanii wa filamu wakiwemo Johari, Monalisa, Irene Uwoya, Odama, Richie pamoja na Jacob Stephan aka JB jana katika viwanja vya Biafra Kinondani jijini Dar es Salaam, wameendesha kampeni ya kuosha magari ili kuchangisha fedha itakayowasaidia waathirika wa ajali za barabarari waliolazwa kwenye wodi ya hospitali ya taifa ya Muhimbili.
Kajala Masanja akiosha gari 
 Kajala Masanja akiosha gari

Akizungumza na Bongo5 kwenye banda la Jaffary Carwash ambapo shughuli hiyo ilipokuwa ikifanyika, JB alisema kama wasanii wana wajibu wa kufanya shughuli za kijamii ili kuisaidia.
“Sisi kama wasanii tunaonyesha tunaweza kutumia nguvu zetu kuosha magari ili kupata pesa za kuwasaidia watu ambao wameathirika kwa ajali za gari. Kwahiyo hii ni sehemu ya wajibu wetu, tunawakaribisha watu waje waoshe magari yao,” alisema JB
JB akiwa na Irene Uwoyo  
JB akiwa na Irene Uwoya
Richie na Kajala wakiwa na mteja wao baada ya kuosha gari lake  
Richie na Kajala wakiwa na mteja wao baada ya kuosha gari lake
Johari na Monalisa wakiosha gari 
Johari na Monalisa wakiosha gari
IMG_5483 
Richie akiosha gari
Monalisa, Odama pamoja na Johari wakisubiria wateja 
Monalisa, Odama pamoja na Johari wakisubiria wateja
Picha Na:- Bongo5

0 comments :

Post a Comment

 

Copyright © 2013. BONGO STARS LINK - Haki zote zimehifadhiwa
Template Modify by Habarizetuleo TEAM
Proudly powered by MAN DUGX