Pata Habari Motomoto za Nje na Ndani ya Nchi kwa njia ya E-mail, Andika E-mail yako hapo chini.


Home » » DIAMOND ACHARUKA BMW LA WEMA!

DIAMOND ACHARUKA BMW LA WEMA!

Ni sheeedah! Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amecharukia gari aina ya BMW 545 alilozawadiwa mwandani wake, Beautiful Onyinye wa Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ ambaye ni Miss Tanzania 2006/07, akipinga gari hilo kupewa na meneja wake, Martin Kadinda.
Gari aina ya BMW 545i alilozawadiwa Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na meneja wake, Martin Kadinda.
DIAMOND ACHANGANYIKIWA
Habari za kipekepeke zilidai kuwa, taarifa ya Kadinda kumpa zawadi ya gari Wema kwenye pati ya bethidei yake Jumapili iliyopita, nyumbani kwake, Kijitonyama, Dar zilimchanganya Diamond na kudai kwamba ni kitu ambacho hakiwezekani kwa maana anamfahamu vyema Kadinda kuwa hana uwezo huo wa kununua BMW la zaidi Sh. milioni 56 za madafu.
Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ akifungua shampeni katika bethidei yake.
Chanzo hicho kiliweka wazi kwamba mkali huyo anayekimbiza na Ngoma ya Mdogomdogo alihamaki baada ya kupata taarifa kuwa siyo yeye peke yake aliyekabidhi zawadi ya gari (Nissan Murano) kwa maana aliamini mwenye zawadi ya gari alikuwa ni yeye tu ambayo ilikuwa ‘surprise’ kwa mpenzi wake huyo.
Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’akipokea funguo ya gari la zawadi kutoka kwa Meneja wake.
BOFYA HAPA KUPATA ‘UBUYU’
 “Unaambiwa Diamond kachanganyikiwa kabisa kusikia Wema kapewa gari, tena BMW na mbaya zaidi aliyempa gari ni Kadinda huku yeye akiamini kabisa zawadi aliyotoa kwa mpenzi wake asingeweza kupata kwa mtu mwingine yeyote, mwenyewe anasema amedhalilishwa kwani hawezi kutoa gari kisha mwanaume mwenzake naye atoe gari,” kilidai chanzo hicho.
Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’
Mpashaji huyo alizidi kufafanua kwamba baada ya kupokea taarifa hizo na kuona kwenye vyombo vya habari na mitandao mbalimbali akiwa nje ya nchi, Diamond alianza kufanya utaratibu wa kurudi nchini akitokea Canada ili kujua vizuri kuhusu undani wa hilo gari.
“Yaani ninyi mtasikia, nakwambia kimenuka maana Diamond aliposikia na kusoma habari za BMW la Wema alianza kufanya utaratibu wa kurudi Bongo ili kupata ufafanuzi zaidi,” kilisema chanzo hicho.
Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’
KADINDA AKOMAA
Kwa upande wake Kadinda ameendelea kusisitiza kwamba yeye ndiye aliyenunua gari hilo na kumkabidhi Wema ikiwa ni michango ya watu wanaomsapoti mwanadada huyo.
Kuhusu gari hilo, watu kibao wamekuwa wakitajwa kulinunua akiwemo mfanyabiashara Mkongo mwenye jina linaloanza na herufi S na mume wa mtu ambaye ni kigogo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) jijini Dar anayetajwa kwa herufi moja ya L.
WEMA VIPI?
Jitihada za kumsikia Wema ziligonga mwamba baada ya simu yake kuita bila kupokelewa na hata alipofuatwa nyumbani kwake hakuwepo hivyo juhudi za kupata lake la moyoni zinaendelea. Stay tuned kwani inavyoonekana nyuma ya pazia ya gari hilo kuna siri kubwa!

0 comments :

Post a Comment

 

Copyright © 2013. BONGO STARS LINK - Haki zote zimehifadhiwa
Template Modify by Habarizetuleo TEAM
Proudly powered by MAN DUGX