Pata Habari Motomoto za Nje na Ndani ya Nchi kwa njia ya E-mail, Andika E-mail yako hapo chini.


Home » » Didas Fashion Amshukia Clouds 112 wa Bongo Movies , Asema Amelamba Ndimu na Kufunguka Mazito

Didas Fashion Amshukia Clouds 112 wa Bongo Movies , Asema Amelamba Ndimu na Kufunguka Mazito


Kupitia ukurasa wa Didasfacion wa Instagram Jana , Mwanadada huyu aishie UK ..Amefunguka Makubwa Kuhusu Bongo Movies hususan Muingizaji Clouds 112...Jisomee Mwenyewe Hapo chini:

"Hahahaha @eshasbuheti na wewe umejitoa kwa ajili yangu kama @stevenyerere2 au?. Mungu huyu analipa hapa duniani. ... Nina mengi ya kuongea alafu mie huwa siongei kwa maneno naongea na evidence. Nina dhambi za mtu natembea nazo na siku kichaa kikinipanda nitazimwaga hadharani, watu wataacha midomo wazi. Watu wanavaa majoho ya mungu kujifanya wema. Na hapo ndio mtajua kwanini movie yangu ya Mateso Yangu Ughaibuni sijaitoa mpaka leo. Nilinyamaza, ila subirini ma evidence yanakuja. Mi mstaarabu ila ni Kiazi kibovu mnooo.

Nasema nimeramba ndimu, nimechoka sasa ni wakati wa kutapika, naomba waandishi wa habari msogee huku kwa page yangu haraka. Maana ule muda muwafaka umekaribia. Mimi ni Mmanyema halisi. Nimekaa kimya nimechoka. Hawa ni wanawake wenzangu. Pole sana @sabrinarupia alafu ninavyo kupenda wewe dada acha tu. It's time.

Jamani mnamuona huyu kaka hapa? Huyu kaka anaitwa Frank kwa wale msio mjua. Huyu kaka ndio alikuwa aje UK kucheza movie ya MATESO YANGU UGHAIBUNI. Na tulisha kubaliana hadi bei maskini na kila kitu kilikuwa poa. Mara ghafla nikapokea simu ya kinafki, na wakati huo mie nilikuwa sijui lolote kuhusu bongo movie. Nikaambiwa huyu kaka ninae taka kumchukua hajui kucheza wala ku direct movie. Nika pampiwa vibaya mnoo mpaka nikatia akili. Frank kokote ulipo naomba unisamehe najua ulikuwa tayari umekuwa na tamaa ya safari ya kuja ulaya, ila waziba rizki wakafanya yao. Wacha naishi hapo. Hii ni intro tu. Hadithi kamili inakuja. Kaeni na ndimu zenu.
-----------------------------------
Clouds 112 Haya uliniita mimi tapeli tena mzulumati, nimekudhulumu million 8 za kuja kucheza movie, ukaenda mpaka kwenye magazeti kusema, nikapigiwa na wenye magazeti, nikawapa ukweli na ushahidi. Tena huu ni mfano tu, ninazo nyingi na za aibu, na bado naendelea. Frank aliniomba nimlipe Tsh 2 million kucheza hiyo movie, nikakubali, wewe ukasema kila kitu utafanya bure ila nikisha uza movie nikufikirie, sasa leo umemfanya @stevenyerere2 kajiuzulu eti kisa kanisaidia uzinduzi, na hela ya PSPF tumekula, huu ni mfano nakuja kumwaga mengi. Ulijitole kila kitu bure uje ulaya, leo umenipaka mavi dunia nzima mimi tapeli, unawafanyia fitna watu wote wanao kaa karibu na mimi. Hii ni haki? Sawa mimi tapeli dhulumati, zote ni njia za kutafuta riziki. Tutafika hata mahakamani. Bado na rudi na mazito zaidi. Ongezeni ndimu


Clouds 112 Nilihangaika kwa nguvu zangu ili nifanye kitu tofauti. Nahangaika na familia yangu. Hata kama movie niliicheza kimaskini, kwani nyie movie zenu mnazicheza kitajiri? Nimeiba, nimenyang'anya, nimekopa kukupandisheni ndege kuja kucheza movie. Kuna matajiri wangapi wana hela zao na visa kupata hawapati? Wangapi wanaingia ubalozini wanakosa visa. Eti unaaenda kumwambia distributors wasichukue movie yangu kisa umedhulumiwa. Unaweza wewe kuzilipa gharama zangu hata kama ni ndogo? Rizki yangu ninavyo itafuta unaijua? Ninavyo hangaika kutafuta maisha na kupigana usiku na mchana unajua? Hujaziba bado rizki yangu ya hiyo movie, mungu akiniandikia hata Kenya watanunua na wata distribute, karoge sasa. Am sick and tired. Nime nyamaza ila nimeshindwa kuvumilia. Wapenzi wangu naomba mnisamehe. Nahangaika kutafuta riziki nile kwa jasho langu na nguvu yangu. Sijakutuma unipe offer yakucheza movie bure ili ukalalamike. Sijamaliza evidence. Mpaka za mapenzi pia. Nakuja nazo

Nadhani Kuna haja ya Kusikia Kutoka Upande wa Pili wa Clouds 112...

0 comments :

Post a Comment

 

Copyright © 2013. BONGO STARS LINK - Haki zote zimehifadhiwa
Template Modify by Habarizetuleo TEAM
Proudly powered by MAN DUGX