Pata Habari Motomoto za Nje na Ndani ya Nchi kwa njia ya E-mail, Andika E-mail yako hapo chini.


Home » » MAUAJI YA WANAWAKE ARUSHA , MAMA FEZZA KESSY NAE ANUSIRIKA KUUWAWA

MAUAJI YA WANAWAKE ARUSHA , MAMA FEZZA KESSY NAE ANUSIRIKA KUUWAWA

WAKATI hofu ya mauaji ya wanawake ikiwa bado imetanda mkoani Arusha, mama mzazi wa mshiriki wa shindano la Big Brother Africa, Feza Kessy ameponea chupuchupu baada ya kuvamiwa na majambazi wawili kisha kuporwa fedha.

Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu kutoka jijini humo, Feza alisema mama yake aitwaye Rose Kessy alikutwa na masaibu hayo mchana wa saa nane, Jumatano iliyopita akiwa hatua chache kutoka nyumbani kwake, eneo la Boma ya Siara, Moshono.

“Watu wawili wakiwa na pikipiki walimsimamisha akiwa garini anarejea nyumbani, wakamteremsha na kuanza kumsachi, wakachukua pochi yake ambayo ilikuwa na shilingi laki tatu ndani. Wakati wanafanya tukio hilo watu walikuwa wanatazama tu bila kufanya lolote.

“Watu wengine walipita na gari wakataka kusimama, lakini wakaonyeshwa bastola na kupewa ishara ya kuendelea na safari. Yaani walikuwa wanafanya wakiwa hawana wasiwasi utafikiri ni askari vile, hivi hapa ndiyo nimerudi kutoka polisi,” alisema mshiriki huyo ambaye pia aliwahi kushiriki shindano la Miss Tanzania miaka ya nyuma.
GPL

0 comments :

Post a Comment

 

Copyright © 2013. BONGO STARS LINK - Haki zote zimehifadhiwa
Template Modify by Habarizetuleo TEAM
Proudly powered by MAN DUGX